Saturday, 19 August 2017

Dirisha la usajili na uhamisho lafungwa Zanzibar,ZFA yasema itazisimamia sheria na kanuni msimu ujao.

Zoezi la usajili na uhamisho visiwani Zanzibar limemalizika Alkhamis Agost 17 nakuenda vizuri na kinachofata sasa nikupitiwa kwa fomu hizo nakuhalalishwa kwa wachezaji kucheza timu husika.


Akizungumza na mtandao huu katibu mkuu wa chama cha mpira wa miguu Zanzibar Muhamed Tedy amesema kumalizika kwa zoezi hilo chama chao kinajipanga kuzipitia fomu hizo.

“Tutarajia kuzipita fomu hizo kesho Jumapili mbele ya viongozi wa vilabu na tutaanza na ligi kuu lengo nikuondoa utata ambao unaweza kujitokeza katika upitishwaji huo wa fomu” alisema.

Ameongeza katika kuendesha zoezi hili watahakikisha wanafuata kanuni na sheria na mwaka huu chama chao kimejipanga kuona wanatekeleza kanuni kwa asilimia zote.

Kuhusu msimu wa 2016-2017 ambao umefikia tamati hapo jana katibu huyo amesema msimu huo umemalizika kwa mafanikio licha ya changamoto ambazo zimejitokeza katika kuendesha ligi hiyo.

Akizungumzia vitendo vya uoangaji wa matokeo ambavyo vilionekana vikijitokeza katika michezo ya ligi kuu soka ya Zanzibar kwa 2016-2017 katibu huyo amesema chama chao kinajipanga kukomesha vitendo kama hivyo.

Msimu wa ligi 2016-2017 ligi kuu soka ya Zanzibar umemalizka jioni ya jana ambapo timu ya JKU kwa mara ya kwanza wametwaa ubingwa wa ligi hiyo huku Zimamoto wakitwaa nafasi ya pili .



No comments:

Post a Comment