Mchezaji Ramadhani
Khamis Muhamed(Neymar) ambae amesajiliwa na Miembeni City kwa mkopo wa mwaka
mmoja akitokea Jang’ombe boys anatarajiwa kujiunga katika mazoezi ya timu yake
hiyo mpya Agost 24 tayari kujianda na msimu ujao wa ligi kuu soka ya Zanzibar.
Neymar ambae ni
miongoni mwa nyota waliong’ara katika msimu wa 2016-2017 ligi kuu soka ya
Zanzibar amepewa mapumziko ya wiki moja kabla yakujiunga na wenzake katika
mazoezi ya timu hiyo ambayo katika msimu huu wa ligi wanacheza ligi kuu soka ya
Zanzibar kwa mara ya kwanza.
Akizungumza na mtandao
huu mkuu wa kitengo cha habari wa Miembeni City Ali Khamis amesema mwalimu
ameamua kumpa mapumziko hayo kwa sababu nyota huyo hakuapata mapumziko kwa vile
alikuwa akiitumikia timu yake katika michezo ya ligi kuu.
“Nikweli tumemsajili
Ramadhani Khamis Muhamed (Neymar) kwa mkopo wa mwaka mmoja kutoka Jang’ombe
boys lakini kwa vile alikuwa akiitumikia timu yake kwenye michezo ya ligi kuu
soka ya Zanzibar iliyomalizika wiki iliyopita tumeamua kumpumzisha hadi hapo Agost
24 na hapo ataanza kujiunga na wenzake katika mazoezi.
Nyota huyo ambae
alikuwa chachu ya mafanikio kwa timu yake katika msimu uliopita wa ligi kuu
soka ya Zanzibar alikuwa miongoni mwa nyota waliounda timu ya combine ya wilaya
ya mjini iliyotwaa ubingwa katika mashindano ya Rolling stone mwaka 2016 huko mjini Arusha.
No comments:
Post a Comment