Saturday, 26 August 2017

ZFA YAZIPITIA FOMU ZA UHAMISHO NA USAJILI,

Kamati tendaji ya chama cha mpira wa miguu visiwani Zanzibar imekutana na vilabu vinavyoshiriki ligi kuu soka kupitia fomu za usajili na uhamisho kwa ajili ya msimu wa 2017-2018.

Akizungumza na waandishi wa habari afisa habari wa chama cha mpira wa miguu visiwani hapa Ali Bakar amesema zoezi hilo limekuja baada yakukamilika kwa zoezi la usajili na uhamisho lililoanza tarehe 17 mwezi wa saba na kukamilika 17 Agosti nakumalizika kwa mafanikio makubwa.

Amesema kuwa zoezi la upitiaji wa fomu hizo limeenda vizuri huku madai kadadha yakasikilizwa kutokana na baadhi ya wachezaji kusajili timu mbili.

Akizungumzia baadhi ya kadhia ambazo zimejadiliwa ni pamoja na suala la mlinzi wa kati wa Miembeni City ambae amesajiliwa na Mlandege Abubakary Ame ambapo kamati tendaji imerizishwa na hoja ya Miembeni City na nyota huyo kuidhinishwa kukipiga katika timu ya Miembeni City.

Sambamba na hayo kamati hiyo pia imesikiliza madai ya Hassan Seif banda ambae pia ameidhinishwa kukipiga katika timu ya Jang’ombe Boys.


Aidha Cheupe amewataka viongozi wa vilabu kufanya maandalizi yaliyo mazuri ilikuifanya ligi kuu kwa mismu wa 2017-2018 iwe ya ushindani na mvuto wa hali ya juu.

No comments:

Post a Comment