Thursday, 24 August 2017

Nitahakikisha najituma kuisaidia Miembeni City kutwaa taji la msimu ujao,Haroun.’

Kiungo hatari wa timu ya Miembeni City , Haroun Abdallah Jabir(Boban)  ameweka wazi kuwa yupo tayari kwa mapambano.
Kiungo wa Miembeni City Haroun Abdallah Boban.
Haroun amedai kuwa moja ya malengo yake ni kuisaidia timu hiyo kutwaa ubingwa wa ligi kuu soka ya Zanzibar kwa msimu ujao.
“Kuanza kwa msimu mpya 2017-2018, kwangu mimi nimejipanga kuisaidia timu yangu kuwa mabingwa msimu ujao na mwenyewe kucheza vizuri kwa kushirikiana na wachezaji wenzangu kwani ushirikiano wetu ndio utatupa hamasa kama wachezaji ya kufanya vizuri na kuisaidia timu yetu kubeba ndoo (ubingwa),” alisema Haroun wakati akizungumza na mtandao wa huu.

Haroun ni mmoja wa viungo wanaokuja kwa kasi kwa sasa Zanzibar, na amekuwa akiwania na vilabu kadhaa visiwani hapa.

Akizungumzia ujio wa Banka ,Guti na Neymar katika kikosi chao  Haroun amesema ujio wa nyota hao kikosini hapo kutasaidia zaidi timu hiyo kufanya vyema huku akisisitiza kuwa kujituma katika mazoezi sambamba na nakuyafanyia kazi maelekezo ya mwalimu mchezoni ndiko kutakakoisaidia timu yao hiyo kufanya vyema katika ligi hiyo.

Sambamba na hayo Haroun amesema kuwa ligi kuu soka ya Zanzibar ni miongoni mwa ligi ngumu dunia kwa vile inashusha timu nyingi ukilinganisha na idadi ya timu shiriki hivyo inahitajia wachezaji wa timu yao kulijua hilo nakujituma zaidi hasa katika kipindi hiki cha maandalizi.


Miembeni City inaendelea kujinoa kujiandaana msimu ujao wa ligi ambapo kwa mara ya kwanza kikosi hicho kinashiriki ligi kuu soka ya Zanzibar.

No comments:

Post a Comment