Chama cha mpira wa miguu visiwani Zanzibar imepokea kwa
masikitiko makubwa kifo cha aliyekuwa daktari wa mwanzi wa timu ya taifa ya
Zanzibar Abdallah Said Mohammed al-maaruf ‘Kuku’, aliefariki dunia Agosti 20,
2017 nyumbani kwake Muembetanga mjini Zanzibar.
Pichani Jeneza lililobeba mwili wa marehemu likitolewa Msikiti
Maiti, Michenzani baada ya kusaliwa. ( picha ndogo kushoto marehemu Abdalla
Said enzi za uhai wake) .Picha kwa msaada wa mtandao wa bin zubery.
|
Akizungumza na mtandao huu makamo wa rais wa ZFA Pemba Ali Muhamed amesema chama chao kimepokea kwa
masikitiko makubwa kifo cha daktari huyo huku akiwataka wote walioguswa na
msiba huo kuwa na subra katika kipindi hiki cha msiba.
Amesema marehemu katika uhai wake alijitolea kwa hali na mali
katika kuwahudumia wachezaji wanapopata matatizo yanayowafanya wasiendelea na
mazoezi.
Ameongeza kuwa marehemu alikuwa akifanya kazi kwa ushirikioano
bila yakujali kuwa anapata chochote au hapati bali alikuwa akihakikisha
anaitumia taaluma yake ipasavyo.
Aidha chama chao kiungana na familia ya marehemu Abdallah Said
katika kipindi hiki cha msiba nakuwaomba wanzazibar kumuombea dunia ili Allah
ampokea akiwa miongoni mwa waja wema.
Marehemu amezikwa jana mchana kijijini kwao Fujoni Wilaya ya
Kaskazini ‘B’ Unguja, ambapo mazishi yake yalihudhuriwa na mamia ya wananchi wa
Zanzibar wakiwemo wanamichezo, madaktari na wafanyakazi wa taasisi mbalimbali
alizozifanyia kazi ikiwemo Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) akihudumu
katika kiwanja cha kufurahisha watoto Kariakoo kilicho chini ya mfuko huo.
Mwenyezi Mungu ailaze roho yake pahala pema Peponi. Amin.
No comments:
Post a Comment