Monday, 21 August 2017

Mfenisini kuelekea Dar es salam kwa matayarisho ya ligi.

Timu ya Mfenisini ambayo imepanda ligi daraja la pili taifa Unguja inatarajiwa kuelekea Tanzania bara kwa ajili ya kambi ya wiki mbili kujiandaa na msimu mpya wa ligi.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo mtandao huu umezipata timu hiyo itakapokuwa Tanzania bara itacheza michezo kadhaa yakirafiki yakujipima nguvu ilikukieka sawa kikosi hicho kwa ajili ya msimu ujao wa ligi.

Mwalimu msaidizi wa timu hiyo Saha ameuambia mtandao huu kwamba baada yakukamilisha kwa usajili wa nyota wapya wa kikosi hicho kinachofata nikukiandaa kikosi chao hicho kwa ajili ya msimu mpya wa ligi ambapo timu itashiriki kwa mara ya kwanza.

Amewataka washabiki na wapenzi wa timu yao hiyo kuwaunga mkono ilikufanya vyema katika msimu mpya wa ligi nakuweza kupanda daraja.





No comments:

Post a Comment