Monday, 21 August 2017

Halid Boffu kitasa cha Miembeni City kuungana na wenzake kesho.

Mlinzi wa kati mpya wa timu ya Miembeni City inayoshiriki ligi kuu soka ya Zanzibar  Khalid Boffu aliesajiliwa akitokea Academy ya Twalipo anatarajiwa kuwasili asubuhi ya kesho akitokea Dar es salam tayari kujiunga na timu yake kwa maandalizi ya msimu ujao wa ligi.
Halid Boffu akijifua katika fukwe  za bahari Boffu atajiunga na wenzake mwishoni mwa wiki hii.

Khalid ambae ni mdogo wa mshambuliaji wa zamani wa timu ya JKU Ruvu Sele Boffu anatarajiwa kuwasili visiwani mnamo majira ya saa tatu asubuhi kwa boti za Azam Marine.

Kwa  mujibu wa taarifa zilizopatika kutoka kwa uongozi wa timu hiyo atakapowasili visiwani hapa nyota huyo atapokelewa na rais wa timu hiyo sambamba na viongozi mbali mbali wa timu na natarajiwa kujiunga katika mazoezi na wenzake kesho kutwa.


Miembeni City tayari imeanza maandalizi kwa ajili yakujindaa na ligi kuu soka ya Zanzibar kwa msimu 2017-2018.

No comments:

Post a Comment