Wednesday, 7 June 2017

Mashindano ya Judo taifa kufanyika July mwaka huu.



Chama mchezo wa judo visiwani Zanzibar kipo katika maandalizi yakufanikisha mashindano ya mchezo huo yanayojulikana kwa jina na Tanzania wit category ambayo yatafanyika mwishoni mwa mwezi wa saba katika uwanja wa Judo Amani.
Wachezaji wa mchezo wa Judo wakiwa katika maonesho ya mchezo huo.


Akizungumza na mtandao huu makamo mwenyekiti wa chama hicho Mohamed Khamis amesema mashindano hayo yatajumuisha vilabu mbalimbali kutoka Tanzania.

Ameongeza kuwa kwa sasa wanamichezo wa mchezo hyo kutoka Unguja na Pemba wanaendelea na mazoezi ya mchezo huo huku akiamini kuwa timu za Zanzibar zinatarajiwa kufanya vyema katika mashindano hayo.
Wachezaji wa mchezo wa Judo wa Zanzibar wakikabidhiwa bendera na makamo mwenyekiti wa baraza Mwalim Khamis.


Amewataka wadau mbali mbali wa michezo kujiunga katika mchezo huo sambamba nakuwasaidia vijana ambao wamejiingiza katika mchezo huo.
Wachezaji wa mchezo wa Judo wakiwa katika mashindano ya mchezo huo.


Akizungumzia changamoto ambazo wanakabiliana nazo katika kuendesha mashindano mbali mbali ya mchezo huo makamo mwenyekiti huyo amesema uhaba wa fedha sambamba na kutokuwa na wadhamini ndiko kunakorejesha nyuma juhudi zao katika kuimarisha mchezo huo.

No comments:

Post a Comment