Thursday, 1 June 2017

DAU,AITA NYOTA 21 UMISETA.

Kocha msaidizi wa timu ya Unguja itakayoshiriki katika Mashindano ya Umoja wa Michezo na Sanaa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) Abdul Wahab Dau ametangaza kikosi cha mwisho kinachojumuisha nyota 21  tayari kwa ajili ya mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika Butimba ,Mwanza June 6, 2017.
 
MLINDA MLANGO WA TIMU YA UMISETA ALEY ALI SULEIMAN.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kocha huyo amesema katika kikosi hicho wamejaribu kuangalia uwezo wa wachezaji husika sambamba na nidhamu ya mchezaji.

Kikosi hicho cha timu ya shule ya sekondari  Unguja kinaundwa na walinda mlango  Aley Ali Suleiman (Ubago) na Ali Makame (Muembe ladu)

                              KIKOSI CHA UMISETA

Huku walinzi wakiwa Ibrahim Abdallah Hamad (Arahman), Abdurahman Seif Bausi (Glorious), Abubakar Khamis (Bububu), Abdul aziz Ameir Khatib (Arahman), Ali Issa Omar (Lumumba),  Ahmed Mohd Shaaban (Nyuki) na Abbas Yahya.

Huku viuongo wakiwa Amani Ali Suleiman (Kiembe Samaki), Ibrahim Faraj “Mess” (Lumumba), Haji Suleiman (JKU Mtoni), Yakoub Kiparo (Langoni), Jamali Ali Jaku “Ozil” (Kinuni) na Eliyasa Suleiman (K-pura).

Huku kwa upande wa washambuliaji Faki Kombo (JKU Mtoni), Mundhir Abdallah (JKU Mtoni), Ali Hassan (Bububu), Walid Abdi “Pato” (Mwera), Ali Mohd Seif (Tumekuja) na Ali Omar (Mwera).

Kikosi hicho kinatarajia kuondoka Visiwani Zanzibar siku ya Jumapili June 3, 2017.


No comments:

Post a Comment