Mkutano mkuu wa chama
cha mpira wa miguu visiwani Zanzibar unatarajiwa kufanyika Jumamos ya April 22
katika kisiwa cha Pemba.
Akizungumzia
maandalizi ya mkuutano huo mbele ya wanahabari afisa habari wa chama cha mpira
wa miguu visiwani Ali Bakar amesema
maandalizi kwa ajili ya mkutano huo yanaenda vizuri.
Ameongeza kuwa kwa
sasa chama chao kipo katika hatua za mwisho zakukalisha utoaji wa posho kwa
wajumbe wa mkutano huo waliopo Unguja ili wakamilishe mahitaji muhimu ya
familia zao.
Aidha amesema baadhi
ya wajumbe wa mkutano huo wanatarajiwa kuondoka Ijumaa kuelekea kisiwani Pemba
kwa usafiri wa baharini huku wengine wakitarajiwa kuondoa Jumamos kupitia
usafiri wa angani.
Akizungumzia ajenda za
mkutano huo amesema ajenda kuu ya kumtano huo ni mabadiliko ya katiba huku
ajenda nyengine ndogondogo zikitarajiwa kujadiliwa katika mkutano.
No comments:
Post a Comment