Kocha mkuu wa timu ya Jamhuri Abdulmutik amesema
wanajipanga kuona wanafanya vyema katika michezo ya hatua ya nane bora ligi kuu
soka ya Zanzibar.
Akizungumza na zenjsport kocha huyo amesema baada yakumaliza
ligi kuu kwa kanda ya Pemba wakiwa vinara wa ligi hiyo kocha huyo amesema kwa
sasa wanaelekeza nguvu zao zote katika hatua ya nane bora ilikuiwakilisha nchi
kimataifa.
Ameongeza kuwa ari katika kikosi chake imekuwa ya
hali ya juu huku viongozi pamoja na beanch zima la ufundi limeandaa mikakati
yakutosha yakuona timu inafanya vizuri katika michezo hiyo ya 8 bora.
Akizungumzia soka katika kisiwani cha Pemba kocha
huyo ambao aliwahi kuifundisha timu ya Kijichi amesema katika kisiwa cha Pemba
kiwango cha soka kipo cha hali ya juu kinachokosekana ni sapoti kutoka kwa
wadau mbali mbali wa soka.
![]() |
Kocha wa timu ya Jamhuri Abdull Kiduu |
No comments:
Post a Comment