Wednesday, 17 May 2017

MCC LAZIMA WAFE ,KISANDU .

Baada ya sare ya tasa dhidi ya timu ya Chuo cha afya Mbweni timu ya chuo cha waandishi wa habari Zanzibar leo hii inajitupa tena dimbani kuoneshana kazi na timu ya chuo cha MCC mtanage ambao utavurumishwa katika dimba la Fuoni mnamo majira ya saa kumi alasiri.
KOCHA WA TIMU YA UANDISHI WA HABARI ZANZIBAR ABUBAKARY HATIBU 

Mtanange huo unatarajiwa kuwa na ushindi kwa pande zote huku kila timu ya ikijinadi kuibuka na ushindi katika mchezo huo.

Kocha wa timu ya chuo cha waandishi wa habari Zanzibar Abubakary Hatibu amesema wamejipanga kuona wanafanya vyema katika mchezo huo huku akitarajia kuwapanga wachezaji ambao wanauwezo wa hali ya juu.
WACHEZAJI WA TIMU YA CHUO CHA HABARI WAKIWA NA KOCHA WAO KISANDU
“Unajua tulitoka sare na afya mchezo ambao ulikuwa na upinzani huku tukiwa pungufu nimerudi mazoezi na vijana wangu nimeyafanyia kazi mapungufu naamini vijana watafanya vyema katika mchezo na MCC”Alisema Kisandu.
KISANDU AKIWA MZIGONI
Akizungumzia vitendo vya utovu wa nidhamu vilivyofanya na mchezaji wake kocha huyo ameelezea kusikitishwa kwake na kitndo hicho huku akiongeza kuwa uongozi wao timu yake umemsimamisha mchezaji huyo na hatamtumia tena katika mchezo wa leo.

No comments:

Post a Comment