Wednesday, 17 May 2017

ZIMAMOTO ,BOYS HAKUNA MBABE ,KIZIMBANI YAIADHIRI MWENGE

Timu ya Jang'ombe boys imelazimishwa sare ya tasa na timu ya Zimamoto ikiwa ni muendelezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar mchezo uliochezwa katika dimba la Amani mjini Unguja.

Katika mchezo huo uliokuwa na ushindani kwa timu zote huku zikiwa na mashambulizi ya zamu hadi kipenga cha muamuzi Mfaume Ally kinapulizwa kuashiria kumalizika kwa mchezo huo hakuna timu iliyoona lango la mweziwe.



Kikosi cha Jang'ombe Boys 

KIKOSI CHA ZIMAMOTO
Katika mchezo uliochezwa katika kiwanja cha Gombani kisiwani Pemba timu ya Kizimbani ikaifungwa timu ya Mwenge magol 2-1.

Ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya nane bora inaendelea kesho ambapo mnamo majira ya saa kumi alasiri katika uwanja wa Amani Taifa ya Jang'ombe itakipiga na timu ya JKU huku katika dimba la Gombani kisiwani Pemba Okapi itakipiga na Jamhuri.

No comments:

Post a Comment