Chama
cha mchezo wa netball Zanzibar (CHANEZA) kimekabiliwa na uchaguzi wa kuwachagua
viongozi wapya ambao watakaoongoza chama hicho cha mchezo wa netball
kuanzia 2017/2021.
Akizungumza
na mtandao huu katibu anaemaliza muda wake wa chama hicho Saidi Mansabu
amesema kamati ya uchaguzi tayari imeshapangwa kinachosubiriwa ni kuratibu timu
ili kujua ni nani anaestahiki kupiga kura katika chama hicho.
Ameongeza
kuwa tayari chama chao kimekutana na viongozi wa baraza la michezo Zanzibar
kutoa baraka za uchaguzi huo sambamba na mrajisi wa vyama vya michezo Zanzibar
ilikufanikisha zoezi hilo kwa ufanisi.
Akizitaja
nafasi ambazo zitagombaniwa kwa upande wa mawilaya ni katibu,mwenyekiti,mshika
fedha pamoja na wajumbe wane huku kwa upande wa taifa nafasi ambazo
zitagombania ni mwenyekiti,makamo mwenyekiti,katibu ,msaidizi katibu sambamba
na mshika fedha.
Akizitaja
sifa za wanastahiki kushiriki katika uchaguzi huo katibu huyo anaemalizia muda
wake amesema kuwa mdau yoyote yule wa mchezo wa net ball ambae amefikia elimu
ya kidatu cha nne nakuwataka wadau mbali mbali wa mchezo huo kujitokeza
kugombania nafasi hizo.
No comments:
Post a Comment