By: Ibny Khamis
Timu pekee ya Zanzibar iliyokuwa ikishiriki katika mashindano ya
Sport Pesa Super Cup Jang’ombe Boys wameaga mashindano hayo baada yakupokea
kipigo cha magol 2-0 kutoka kwa timu ya Gor Mahia kutoka nchi Kenya.
![]() |
Wachezaji wa timu ya Jang'ombe boys wakitoka katika uwanja wa uhuru wakiwa na hudhuni baada yakupokea kipigo cha magol 2-0. |
Boys ambao walishiriki mashindano hayo wakiwa timu alikwa
wanatarajiwa kurudi visiwani leo hii.
Akizungumza na mtandao huo rais wa timu hiyo Ali Othman amesema
wameaga mashindano hayo kwa masikitiko huko akisema vijana wake walipoteza
mchezo huo kutokana na kuishiwa na
nguvu.
Ameongeza mashindano yale yameleta heshima na motisha kubwa kwa vijana wake
na wanarudi zanzibar kujiandaa na michezo ya hatua ya nane bora yanayotarajiwa
kuanza baada ya kumalizika mfungo wa sunna ya sita.
“Unajua mashindano yale yameongeza motisha zaidi kwa vijana
wangu na hamu yakuiwakilisha nchi kimataifa imeongezeka tunarudi kujiandaa na
mzunguko wa pili ambao unaanza mara tu baada ya mfungo wa sunna ya sita
,tunahitaji nafasi zidi yakuwakilishi hivyo tunaelekeza nguvu zetu katika ligi
ya nyumbani “alisema Kibichwa.
Kuhusu kutakiwa kwa mlinzi wao wa kati Ali Humud balii na timu
ya Simba rais huyo amesema ni mapema mno kulizungumzia suala hilo lakini
ukifika muda wake kila kitu kitawekwa wazi.
"Ibny hakuna kitu cha siri katika soka hili suala kama lipo litakuja juu tu wala usijali tumuombe mungu kama lipo liwe la heri ili kijana wetu atoke zaidi katika soka na sisi boys kila tukiona vijana wetu wanatoka kisoka ndo tunakuwa na furaha "alimaliza kibichwa.
Nyota wa Jang'ombe
Boys waliwakilisha katika mchezo huo ni Ruga Hasham, Said Ibrahim, Amour Firdaus, Chandika Ibrahim, Ally
Sammad, Abdi Kassim ‘Babbi’, Abdallah Rashid/Ali Aboukabar dk79, Makame
Khamis, Juma Hafidh, Ali Shekha na Abdallah Hussein.
No comments:
Post a Comment