Saturday, 3 June 2017

MIEMBENI CITY YAZINYEMELEA SAINI ZA NYOTA TOKA LIGI KUU TANZANIA BARA.


Wakiwa katika mikakati yakukiimarisha kikosi chao baada yakupandisha ligi kuu soka ya Zanzibar kwa msimu wa 2017-2018 uongozi wa timu ya Miembeni City wamepania kufanya usajili wa nguvu ilikuimarisha kikosi chao.
MKURUGENZI WA UFUNDI WA TIMU YA MIEMBENI CITY AKIZUNGUMZA NA WASHAMBULIAJI WA TIMU HIYO IBRAHIM ABDALLAH(MKOKO) NA  SAID PAMBA



Kwa mujibu wa taarifa ambayo mtandao huu umezipata ni kwamba uongozi wa timu hiyo wapo katika mazungumzo na nyota kadhaa ambao katika msimu uliopita walizitumikia timu zinazoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Afisa habari wa timu hiyo Ali Khamis ( Ibny) amesema mara baada yakumalizika kwa ligi daraja la kwanza taifa na timu yao kumalizakwa mafanikio makubwa mwalimu wa timu hiyo sambamba  na beanch zima la ufundi lilitoa mapendekezo yake ya nafasi gani zijazwe na tayari uongozi wa timu unayafanyia kazi mapendekezo hayo.
RAIS WA TIMU YA MIEMBENI CITY SEIF KOMBO ALIEVA NGUO NYEUSI AKISHUHUDIA NAHODHA WA TIMU YAKE HABIBU ALI AKIKABIDHIWA KOMBE LA USHINDI WA LIGI DARAJA LA KWANZA TAIFA UNGUJA

“Unajua tumemaliza msimu kwa mafanikio nakupandisha timu kinachofanyika kwa sasa nikuona tunafanya usajili wa maana kulingana na daraja ambalo timu itacheza na mchezaji yoyote yule ambae timu itakuwa inamuhitaji tutamsajili hata kama atakuwa anacheza  Yanga,Simba,Azam na timu nyengine hapa Tanzania tutamsajili nakuitumikia Miembeni City”Alisema Ibny.

Ameongeza kuwa wamepania kukiimarisha zaidi kikosi chao ili kiwe bora zaidi nakuleta upinzani wa hali ya juu huku wakijua kuwa ligi ambayo timu imepanda ni nguvu na yenye  ushindani hivyo lazima kukiimarisha kikosi chao kiweze kupambana.
Kuhusu suala la ligi ndogo msemaji huyo amesema hilo suala ni la chama cha soka hivyo yeye hawezi kulizungumzia bali wanachojua wao ni kukiimarisha kikosi chao ili kiwe imara na kiweze kuwa cha ushindani zaidi.
KHAMIS MCHA VIALI 


Miembeni City ambayo imefanikiwa kutinga ligi kuu soka ya Zanzibar baada yakutwaa ubingwa wa ligi daraja la kwanza taifa Unguja kwa kushinda katika michezo yake yote ya hatua ya nne bora.




No comments:

Post a Comment