Saturday, 3 June 2017

TUMIE FURSA YA UNAACHAMA WA CAF KUVITANGAZA VIPAJI VYENU KIMATAIFA,BI CHUMU.

Wanamichezo visiwani Zanzibar wametakiwa kuvitumia vipaji vyao ipasavyo katika kuitangaza Zanzibar kimataifa sambambana kujikwamua kimaisha.
WANAMICHEZO WA ZANZIBAR WAKIMSIKILIZA NAIBU WAZIRI WA HABARI ,UTALII,UTAMADUNI NA MICHEZO CHUMU KOMBO HAYUPO PICHANI.


Ushauri huo umetolewa na naibu waziri wizara ya habari utamaduni,utalii na michezo wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Chumu Kombo wakati alipokuwa akizungumza na wanamichezo wa Zanzibar wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya Umiseta.

Amesema kuwa kwa sasa Zanzibar imepatiwa uanachama wa shirikisho la soka barani Afrika hivyo umefika wakati sasa kwa vijana kuitumia fursa hiyo ipasavyo ilikuweza kujikwamua na umasikini kupitia vipaji vyao.

Nae naibu waziri wizara ya elimu na mafunzo ya amali Zanzibar Mmanga Mjengo amewataka wanamichezo hao kuzingatia suala zima la nidhamu watakapokuwa katika michezo hiyo.

Jumla ya wanamichezo 135 kutoka Unguja na Pemba wameondoka Unguja mchana wa leo kuelekea Tanzania bara kushiriki katika mashindano ya  michezo  na sanaa skuli  za secondary Tanzania Umiseta.




No comments:

Post a Comment