Saturday, 3 June 2017

TUITUMIE ZAFCA KUBORESHA TAALUMA ZETU,KOCHA MUU.

Makocha wa soka Visiwani Zanzibar wameshauriwa kuchukua fomu zakujiunga na uanachama wa chama cha Makocha visiwani Zanzibar ili kuendana na matakwa ya shirikisho la soka barani Afrika.
Mustafa Hassan katibu msaidizi ZAFCA


Ushauri huo umetolewa na katibu msaidizi wa chama cha makocha Zanzibar Mustafa Hassan wakati alipokuwa akizungumza na Mtandao huu nakusema kuwa kujiunga katika chama hicho kutasaidia kutumia fursa zitakazokuja kwa ufanisi mkubwa.


“Nawaomba makocha wenzangu waje kujiunga na ZAFCA, mana huko tunakokwenda ni kugumu mno, baada ya ZFA kuwa mwanachama wa CAF, tumetakiwa makocha wote wajinge na chama chao ili watambuliwe na ZFA na hapo ndipo utapata fursa ya kusoma kozi mbali mbali za makocha”. Alisema Mustafa.

Ameongeza kuwa mafunzo yote ya ukocha ambayo yatakuja visiwani yatatoa kipaumbelea kwa wale ambao watakuwa ni wanachama wa chao hicho

No comments:

Post a Comment