Friday, 2 June 2017

JANG'OMBE BOYS KUIFUATA TIKETI YAKUCHEZA NA EVERTON .

Timu ya Jang’ombe inatarajiwa kuondoka visiwani Zanzibar asubuhi ya kesho kuelekea Tanzania bara ambapo itashiriki katika mashindano ya Sport Pesa Super Cup.
KIKOSI CHA JANG'OMBE BOYS AMBACHO KITAONDOKA KESHO KUELEKEA TANZANIA BARA KATIKA MASHINDANO YA SPORT PESA SUPER CUP.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na rais wa timu hiyo Ali Othman wanandinga hao wanatarajiwa kuondoka mnamo majira ya saa tatu asubuhi kwa boti za Azam Marine.
JANG'OMBE BOYS

Boys ambao wamepangwa kucheza Jumanne ,June 6, 2017 na  Gor mahia kutoka nchini Kenya wanaenda katika mashindano hayo wakihitaji ushindi.
Akizungumzia hali ya kikosi chao rais wa timu hiyo amesema kikosi chao kipo katika hali nzuri huku wakitarajia kufanya vyema katika mashindano hayo.
Mshindi katika mashindano hayo anatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Everton inayoshiriki ligi kuu soka ya Uengereza.

RATIBA YA AWALI YA MASHINDANO HAYO
Jumatatu 5/6/2017
Singida united Vs FC leopard
Yanga Vs Tusker fc

Jumanne 6/6/2017
Simba Vs Nakuru All Star

Jang`ombe boys vs Gor mahia

No comments:

Post a Comment