Sunday, 4 June 2017

RIADHA ZANZIBAR WAUMIZWA NAKUTOJUMUISHWA KATIKA TIMU YA TANZANIA YA RIADHA.


Kufuatia kutoitwa kwa wanariadha wa Zanzibar kujumuika na wenzao wa Tanzania bara katika timu ya taifa ya riadha ya vijana ya Tanzania baadhi ya walimu wa mchezo huo visiwani wameelezea kuumizwa na kitendo hicho.

Akizungumza na mtandao huo mmoja wa makocha hao Abdallah Juma Abeid amesema kutokana na kiwango kilichooneshwa na wanariadha wa Zanzibar katika mashindano ya riadha ya Afrika Mashariki na Kati yaliyomalizika hivi karibu suala lakutoitwa katika timu ya taifa ya Tanzania kunarejesha nyuma juhudi zao.
Ameongeza kuwa kutoka na ushindi ambao wameupata wachezaji hao lazima wachezaji hao walikuwa wajumuishe katika orodha za wachezaji ambao watashiriki katika mashindano ya riadha ya Afrika sambamba na Dunia.
“Unajua wachezaji tayari wameitwa na tayari wanatarajiwa kuenda katika kambi yakujiandaa na mashindano ya Afrika nchini Kenya lakini hakuna mchezaji hata mmoja wa Zanzibar alieitwa katika timu hiyo jambo ambalo linarejesha nyuma juhudi zao”alisema  Abdallah.
Aidha amesema kuwa mashindano ya riadha ya Afrika kwa vijana yanatarajiwa kufanya nchini Algeria mwanzoni mwa mwezi wa sita na yale ya dunia yakitarajiwa kufanyika nchini Kenya mwezi wa saba.

Akiwataja vijana ambao walifanya vyema katika mashindano ya Afrika Mashariki na Kati ambao wanastahiki kuwepo katika timu hiyo ni pamoja na Omar Rashid(Burning),Kazija Hassan,Hafidh Abdallah na Dahala Musilihi Dahala ambao walitwaa medal ya dhahabu katika mashindano hayo lakini hawajajumuishwa katika timu hiyo ya taifa ya Tanzania.

No comments:

Post a Comment