Saturday, 17 June 2017

Uongozi Miembeni City, kutoa mkono wa Idd kwa nyota wake.

Bodi ya wakurugenzi wa timu ya Miembeni City kesho wanatarajiwa kukutana na nyota wanaokipiga katika kikosi hicho kwa lengo lakutoa mkono wa Idd kwa nyota wao hao.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na rais wa timu hiyo Seif Kombo imesema kwamba huo ni utaratibu ambao upo katika kikosi chao hicho kila ifikapo mwishoni mwa mwezi mtukufu wa Ramadhani kuwakusanya nyota wao hao kwa lengo lakuwapatia fedha ilikujitafutia huduma ambazo zitawasaidia kwa ajili ya Idd.

Ameongeza kuwa baada ya kikao cha bodi ya wakurugenzi wa timu hiyo kilichokutana asubuhi ya leo kimekubaliana kutoa fedha hizo kwa nyota wao ilikufanya nyota hao kuwa na siku njema ya Idd.

“Huu ni utaratibu ambao tumejiekea kuwapatia fedha nyota wetu kila ifikapo mwishoni mwa mwezi mtukufu wa Ramadhani ilioneshana upendo kati ya viongozi wa timu na wachezaji wetu waliopo katika kikosi chetu hicho”alisema rais huyo.

Akizungumzia maandalizi ya kikosi chao kuelekea msimu ujao wa ligi rais huyo amesema baada yakumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani wataanza maandalizi ya msimu mpya  wa ligi kulingana na maelekezo ya mwalimu wa kikosi chao hicho.


Kuhusu suala la usajili rais huyo amesema  mwalimu amependekeza nafasi ambazo zinahitaji kufanyiwa marekebisho sambamba na wachezaji ambao waache katika kikosi hicho kwa ajili ya msimu ujao wa ligi.

No comments:

Post a Comment