Monday, 19 June 2017

VILABU KUKUTANA KUJADILI MFUMO WA LIGI KUU KWA MSIMU 2017-2018.

Viongozi wa vilabu 28 vya soka vinavyoshiriki ligi kuu soka ya Zanzibar vinatarajiwa kukutoka katika ukumbi wa mikutano uwanja wa Gombani kisiwani Pemba kujadili njia ambazo zitatumika kupatikana kwa timu 12 zitakazoshiriki ligi kuu kwa msimu wa 2017-2018.
Makamo wa rais wa ZFA Ali Muhamed.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na msemaji wa chama cha mpira wa miguu Ali Bakar mbele ya wanahabari imesema  viongozi hao wanatarajiwa kukutana July ,8 mwaka huu.

Cheupe amesema kuwa mkutano mkuu wa chama cha mpira wa miguu visiwani uliokutana mwezi mmoja uliopita umebariki msimu ujao wa ligi uwe na timu 12 hivyo kukutana na vilabu husika ndiko kutakapotoa fursa ya njia gani ambayo itapelekea kupatikana kwa vilabu vinavyohitajika katika ligi hiyo.


Ameongeza kuwa maamuzi ambayo yatafikiwa katika mkutano huo wa viongozi wa vilabu ndiyo yatakayopelekwa katika mkutano mkuu wa chama hicho nakupelekea kupatikana kwa timu zitakazoshiriki katika michezo hiyo.

No comments:

Post a Comment