Monday, 19 June 2017

MACHUPA KUENDESHA KOZI YA MAKOCHA WA MAGOLIKIPA.

Chama cha mpira wa miguu visiwani Zanzibar kinatarajiwa kuandaa kozi ya ukocha wa magolikipa kozi ambayo inatarajiwa kufanyika Juni ,28 mwaka huu.

Mkufunzi wa kozi ya makocha wa makipa Saleh Machupa.

Akizungumza na waandishi wa habari msemaji wa chama cha mpira wa miguu visiwani Ali Bakar amesema kozi hiyo ya ukocha wa magolikipa inatarajiwa kuendeshwa na mkufunzi anaetambuliwa na shirikisho la soka barani Afrika CAF, Saleh Machupa.

Ameongeza kuwa kozi hiyo itajumuisha makocha wa magolikipa wa vilabu vinavyoshiriki ligi kuu soka ya Zanzibar,ligi daraja la kwanza taifa na la pili taifa.


Aidha amesema kuwa katika msimu ujao wa ligi timu ambayo haitakuwa na kocha wa magolikipa mwenye cheti timu hiyo itaondolewa katika mashindano kulingana na kanuni ambayo itatumika katika mashindano hayo.

Amefafanua kuwa kozi hizo za makocha wa magolikipa itakuwa ikiendeshwa kila kipindi kutokana na mahitaji yananafasi hizo visiwani

No comments:

Post a Comment