Monday, 19 June 2017

Bushir ,apendekeza nyota 4,Mwadui fc,wawili wakitokea Zanzibar.

Aliyekuwa kocha wa timu ya KMKM inayoshiriki ligi kuu soka ya Zanzibar Ali Bushir Mahmoud amekishauri chama cha mpira wa miguu visiwani kutumia njia za busara katika kufanikisha kupatikana kwa timu 12 zitakazoshiriki ligi kuu soka kwa msimu ujao wa ligi.
Kocha wa timu ya Mwadui Ali Bushir Mahmoud.

Bushir ameyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na mtandao huu nakusema kuwa busara kwa viongozi wa vilabu sambamba na wale wa ZFA inahitajika katika kufanikisha suala hilo.

Ameongeza kuwa endapo viongozi wa vilabu sambamba na wale wa ZFA wataeka pembeni masilahi binafsi nakuangalia zaidi manufaa ya taifa vilabu 12 vitapatikana bila hata ya malumbano na migogoro.

Kuhusu suala la vilabu vilivyopanda ligi kuu soka ya Zanzibar kwa msimu wa 2017-2018 kocha huyo amesema si busara vilabu hivyo kuviunganisha na vile vilivyopo ligi kuu katika msimu uliopita katika mchako wakutafuta timu hizo bali zijumuishwe kucheza ligi kuu kama kanuni iliyoendesha mashindano inavyosema.

“Mimi nasikia mijadala mingi sana kama kuna ligi ndogo tusubiri tuone kama itakuwepo hiyo ligi ndogo au vilabu na viongozi wa ZFA watakuja na njia nyengine zakupatikana timu 12 mimi binafsi suala lakuchezwa ligi dogo kwangu sioni kama kuna tatizo sana ila hizi timu kama Miembeni City na Charawe sambamba na zile mbili za kule Pemba ambazo zimepanda ligi kuu kwa msimu wa 2017-2018 kwa mujibu wa kanuni sioni sababu yakujumusha hapa ,kama watacheza na wenyewe kwa wenyewe waliopanda kutafuta timu mbili zakupanda badala ya nne nahisi inaweza kuwa njia sahihi lakini kuwacheza na wale waliopo kwenye ligi si jambo sahihi kwa muono wangu”alisema kocha huyo.

Aidha amewaomba viongozi wanaongoza soka la Zanzibar kusimamia sheria zinazoongoza soka nakujaribu kufanya  mazungumzo na baadhi ya makampuni ilikuona haja yakufadhili ligi kuu soka ya  visiwani ilikuongeza mvuto na ushindani katika ligi hiyo.

Akizungumzia ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara akiwa na timu ya Mwaduwi yaShinyanga kocha huyo amesema ligi hiyo inaushindani zaidi ukilinganisha na ile ya nyumbani Zanzibar huku akiongeza kuwa ushindi umeongezekana zaidi kutokana na ufadhili ambao upo katika ligi yao.

Amefafanua kuwa tayari ameshafanya mazungumzo na nyota wawili wanaokipiga ligi kuu soka ya Zanzibar ambapo ni mlinda mlango sambamba na kiungo mkabaji ambapo bado hajataka kutaja majina ya nyota hao kwa vile mazungumzo kati ya viongozi wa Mwadui na nyota hao bado hayajafanyika.

No comments:

Post a Comment