Wednesday, 21 June 2017

SINA MPANGO WAKUONDOKA MIEMBENI CITY,PRINCE,

Mshambuliaji nyota wa timu ya Miembeni City,Muhamed Vuai Prince amesema kwa sasa hana mpango wakuhama katika kikosi hicho huku akielekeza nguvu zake kuitumikia timu hiyo katika msimu ujao wa ligi.
 
Mshambuliaji wa timu ya Miembeni City ,Muhamed Vuai Prince akiwa katika mizunguko yake katika mitaa ya Vuga mjini Unguja.
Prince ameyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na mtandao huu nakusema kuwa baada yakuisaidia timu hiyo kupanda ligi kuu soka ya Zanzibar kwa msimu wa 2017-2018 kwa sasa anajipanga kuona anaisaidia timu yake kutwaa ubingwa wa ligi hiyo ambapo watashiriki kwa mara ya kwanza.

“Tulikuwa na msimu nzuri tumefanikisha kuipandisha timu ligi kuu nashukuru nilikuwa chachu ya ushindi katika timu yangu kwa sasa najipanga kuona nafanya zaidi kile nilichokifanya katika msimu uliopita ilikuisadia timu yangu kutwaa ubingwa wa ligi kuu soka ya Zanzibar katika msimu wa 2017-2018 ambao timu itashiriki kwa mara ya kwanza”Alisema Prince.
 
Muhamed Vuai Prince akiwajibika katika moja ya michezo ya ligi daraja la kwanza taifa Unguja.
Ameongeza kuwa licha yakuwepo kwa taarifa kadhaa juu ya nyota huyo kuondoka katika kikosi hicho,mshambuliaji huyo amesema yeye binafsi huzisikia taarifa hizo kutoka kwa watu bali hajafanya mazungumzo na timu yoyote huku kwa sasa akili yake akiielekeza katika kuisadia timu yake hiyo kufanya vyema katika msimu ujao wa ligi.

Amefafanu kuwa mkataba wake wa Miembeni City umesalia misimu miwili hivyo haoni haja yakufanya mazungumzo na timu yoyote ile bali lililobakia kwa sasa nikufanya mazoezi kwa bidii kubwa kwa ajili ya msimu mpya wa ligi.

Ameelezea kufurahishwa kwake na mazingira yaliyopo katika kikosi hicho huku akifurahishwa na mashirikiano aliyoyapata katika msimu wake wa kwanza akiwa na kikosi hicho kutoka kwa wachezaji wenzake sambamba na uongozi wa timu hiyo.

Prince ambae amemaliza msimu wa ligi 2016-2017 akiwa kinara wakufumania nyavu katika kikosi cha Miembeni City kumekuwa na taarifa yakutakiawa na vilabu kadhaa visiwani ikiwemo taifa ya Jang’ombe.




No comments:

Post a Comment