Licha yakupokea kipigo
cha tatu mfululizo kocha mkuu wa timu ya Miembeni City asema ameridhishwa na
kiwango kilichooneshwa na vijana wake katika mchezo dhidi ya JKU.
Akizungumza na mtandao
huu mara baada ya mchezo wa timu hiyo na JKU kocha wa timu hiyo Muhamed Seif
King amesema ameona mabadiliko makubwa katika kikosi chake katika kila mchezo
na anamatumaini makubwa yakufanya vyema katika michezo ijayo.
Ameongeza kuwa kikosi
chake ni kigeni katika ligi lakini pia kinaunda na vijana ambao ni wanagenzi
lakini katika kila mchezo wameonekana wakibalika jambo ambalo yeye kama mwalimu linampa matumaini na anaamini watafanya vyema katika michezo ya mbeleni.
Miembeni City ambayo
tayari imeshashuka dimbani mara tatu nakupoteza katika michezo yote mitatu
ambapo walifungwa na Polis gol 1-0,kisha mafunzo 1-0 na jana kukubali kipigo
cha idadi kama hiyo cha goli 1-0 kutoka kwa mabingwa watetezi wa ligi hiyo JKU.
No comments:
Post a Comment