Tuesday, 10 October 2017

ZFA YARIZISHWA NA MICHEZO YA MZUNGUKO WA KWANZA LIGI KUU SOKA ,ZANZIBAR.

Michezo ya mzunguko wa kwanza ligi kuu soka ya Zanzibar sambamba na ligi daraja la kwanza taifa Unguja imeenda vizuri huku ushindani ukionekana wa hali juu ka timu shiriki.

Hayo yameelezwa na katibu mkuu wa chama cha mpira wa miguu visiwani Zanzibar Muhamed Hilal Tedy wakati alipokuwa akizungumza na mtandao huu nakusema kuwa ushindani ulioneshwa na timu husika unaashiria maandalizi mzuri kwa timu hizo.

Ameongeza kuwa chama chao kitasimamia kanuni na sheria zakuenda mashindano hayo ikiwemo lessen kwa walimu wanaofundisha timu shiriki ambapo kanuni inahitaji mwalimu kuanzia lessen B.

Akizungumzia timu ambazo hazijafata kanuni na sheria ya mashindano hayo katibu huyo amesema chama chao kinajipanga kuwapatia adhabu kwa mujibu wa sheria na kanuni.

Kuhusu suala la waamuzi ambao wamechezesha michezo hiyo nakulalamikiwa katibu huyo amesema tayari chama chao kimeshafanya mazungumzo na viongozi wa waamuzi hao kuhusu suala hilo.

Aidha amewataka wadau na wapenda mchezo wa soka kujitoka kwa wengi viwanjani ilikuunga mkono timu zao.


Ligi kuu soka ya Zanzibar inatarajiwa kuendelea October 15 ,ambapo michezo miwili itavurumishwa siku hiyo mnamo majira ya saa 8 mchana JKU itakipiga na timu ya Chuoni huku mnamo majira ya saa kumi alasiri Miembeni City itakipiga na Mafunzo.

No comments:

Post a Comment