Wednesday, 25 October 2017

Mzunguko wa nne ligi kuu soka Zanzibar kituo cha Unguja kuanza kesho,Miembeni City kuwakaribisha Chuoni FC.

Baada yakuenda mapumzikoni kwa takribani siku mbili ligi kuu soka ya Zanzibar kituo cha Unguja inatarajiwa kuendelea tena hapo kesho kwa kuanza michezo ya mzunguko wa nne.

Ambapo hapo kesho mtanange mmoja utavurumishwa katika kiwanja cha Amani mjini Unguja mnamo majira ya saa kumi alasiri ambapo timu ya Chuoni itajitupa katika kiwanja cha Amani kuoneshana kazi na timu ya Miembeni City.

Chuoni inashuka katika kiwanja cha Amani mjini hapa wakiwa na alama 4 huku Miembeni City wenyewe wakijitupa katika mchezo huo wakiwa na rekodi mbaya yakupoteza michezo mitatu mfululizo.

Michezo mengine ya mzunguko huo wa nne ya ligi kuu soka ya Zanzibar inaendelea kesho kutwa Jumamos ambapo mitanange miwili itavurumishwa mnamo majira ya saa nane mchana Taifa ya Jang’ombe itakipiga na JKU  huku mnamo majira ya saa kumi alasiri KVZ inamenyana na Mafunzo.

Ikiwa ligi hiyo inaingia mzunguko wa 4 jioni ya kesho mpaka sasa timu ya KVZ inaongoza ligi hiyo wakiwa na alama 9 wakifuatiwa na JKU wenye alama tisa tofauti yao ikiwa ni magol yakufungwa nanakufunga.

Ratiba kamili ya michezo ya mzunguko 

IJUMAA
27/10/017
22
MIEMBENI CITY
VS
CHUONI
SAA 10:00 ALS AMAAN
J’MOSI
28/10/017
23
TAIFA YA J/MBE
VS
JKU
SAA 8:00 MCH AMAAN
J’MOSI
28/10/017
24
KVZ
VS
MAFUNZO
SAA 10:00 ALS AMAAN
J’PILI
29/10/017
25
KIPANGA
VS
POLISI
SAA 8:00 MCH AMAAN
J’PILI
29/10/017
26
KMKM
VS
ZIMAMOTO
SAA 10:00 ALS AMAAN
J’TATU
30/10/017
27
BLACK SAILORS
VS
CHARAWE
SAA 8:00 MCH AMAAN
J’TATU
30/10/017
28
JANG’OMBE BOYS
VS
KILIMANI CITY
SAA 10:00 ALS AMAAN

No comments:

Post a Comment