Wednesday, 25 October 2017

Simba yazidi kuitafutia kasi Yanga na mvua yao.

Wekundu wa msimbazi Simba wanaendelea kujinoa visiwani Zanzibar kwa ajili yakujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara dhidi ya mahasimu wao Yanga mchezo ambao utavurumishwa Jumamosi Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.


Simba ambao wapo visiwani wanafanya mazoezi yakujiandaa na mchezo huo katika kiwanja cha Amani kwa wakati wa asubuhi na katika dimba la jeshini jioni kwa baadhi ya siku.

Ikiwa simba ikiendelea na mzoezi yakujiandaa na mahasimu wao Yanga mshambuliji wachezaji wao waliokuwa majeruhi mshambuliaji John Bocco na kiungo Mohammed ‘Mo’ Ibrahim wameonekana wakifanya mazoezi ya nyota wenzao kuashirikia kuwa tayari kuikabilia Yanga.



Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na afisa habari wa timu hiyo wekundu hao wa msimbazi wanatarajiwakuondoka visiwani hapa Jumamosi asubuhi kuelekea Tanzania bara kwa mchezo huo.

No comments:

Post a Comment