Thursday, 26 October 2017

ZFA yaridhishwa na maendeleo ya soka la wanawake visiwani.

Chama cha mpira wa miguu visiwani Zanzibar kimeelezea kuridhishwa kwake na hamasa  uliojitokeza kwa timu za wanawake zinazoshiriki ligi dogo ya kinamama inayoendelea katika kiwanja cha Amani mjini Unguja ambapo lengo nikutafuta wachezaji 20 watakaounda timu ya taifa ya wanawake itakayoshiriki katika mashindano ya kina mama kule nchini Rwanda.

Akizungumza na mtandao huu katibu wa chama cha mpira wa miguu Zanzibar Muhamed Ali Hilal Tedy amesema michezo hiyo inayoendelea visiwani hapa tayari makocha waliopewa jukumu lakutafuta wachezaji wanaendelea kufanya kazi hiyo.

Ameongeza kuwa katika michezo iliyochezwa vijana kadhaa wameonesha viwango vya hali ya juu na kinachosubiriwa kwa sasa ni makocha waliopewa jukumu kumaliza kazi yao nakutangazwa watakaobahatika kuitwa katika timu ya taifa ya wanawake.


Ameongeza kuwa tayari chama chao kimepokea majina ya wachezaji watano kutoka Pemba ambao wataungana na 15 kutoka Unguja kutangazwa kikosi kamili.


Ameongeza kuwa mara baada yakutangazwa kwa kikosi hicho kocha aliepewa dhama yakukinoa kikosi hicho ataanza majukumu yakukiandaa kikosi kabla yakuondoka kuelekea katika mashindano ya Afrika mashariki na kati kwa upande wa kina mama yanayotarajiwa kufanyika Rwanda mapema mwezi ujao.

No comments:

Post a Comment