Mashindano ya
vijana Central league wilaya ya mjini Unguja yamezinduliwa rasmini asubuhi ya
leo katika kiwanja cha Amani mjini Unguja kwa mchezo kati ya timu ya Aman
Academy na timu ya Mpira Pesa.
![]() |
Rais wa Raska zone Ali Mkanga akisalimiana na muamuzi wa mchezo kati ya timu ya Amani Academy na Mpira Pesa Abubakary Khatibu mchezo ambao umemalizika kwa sare yakufungana goli 1-1. |
Katika mchezo
huo ambao ulikuwa na ushindani kwa pande zote timu hizo zimetoka sare
yakufungana goli 1-1.
Akizungumza katika
hafla ya ufunguzi wa mashindano hayo mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu
wilaya ya mjini Unguja Hassan Haji Hamza amemewataka walimu wanaofundisha soka
la vijana kuachana na vitendo vya unyanyanyasaji watoto sambamba na kuwaingilia
kinyume na maumbile.
![]() |
Viongozi wa kamati ya mashindano ya vijana wilaya ya mjini wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmini katika mchezo wa ufunguzi wa mashindano hayo Ali Mkanga. |
Amesema kwa
kipindi cha hivi karibuni kumekuwa na malalamiko mengi kwa baadhi ya makocha
kushiriki katika vitendo hivyo jambo ambalo linahitajika kupingwa kwa nguvu
zote.
Amesema endapo
chama chao kitapata uhakika wa tuhuma hizo hatua kali watamchukulia muhusika
huku akilitaka jeshi la polisi visiwani kufuatilia kwa umakini mkubwa tuhuma
hizi ili kama zipo ziwezekupatiwa ufumbuzi.
Kwa upande
wake rais wa Raska zone Ali Mkanga amewataka vijana kujituma katika michezo
kwani michezo ni ajira.
No comments:
Post a Comment