Sunday, 29 October 2017

NYOTA REAL KIDS FC,WAPIMWA AFYA ZAO ,TAYARI KWA MICHEZO YA VIJANA YALIYOFUNGULIWA JUMAMOS OCTOBER 28.

Katika kuhakikisha wanaepusha matatizo ya kiafya kwa wachezaji wao wawapo uwanjani uongozi wa timu ya  Realkdis Fc inayoshiriki ligi madaraja ya vijana nadani ya wilaya ya ya mjini Unguja imewafanyia vipimo vya afya nyota wao ilikujua matatizo yanayowakabili nyota hao.

Akizungumza nasi katibu wa timu hiyo Nassor Abdaallah amesema lengo kuu lakufanya hivyo nikujua afya za nyota wa sambamba na kuepusha matatizo ambayo yanaweza kujitokeza kwa wachezaji ambao kwa mujibu wa afya zao hawastahiki kucheza mpira.

Aidha ameishukuru timu ya maktari ambayo imefanya kazi hiyo kwa kushirikia na uongozi wa timu hiyo nakusema zoezi hilo la upimaji afya kwa wachezaji wao litakuwa likifanya kila muda ilikulinda afya za wachezaji wao nakuwataka wachezaji wa timu hiyo kufuata ushauri waliopewa na madaktar baada yakupima afya.


"Tunawashukuru timu ya madaktari kwa kushirikiana na uongozi kuhakikisha kuwa zoezi hili la upimaji wa afya limekwenda vizuri na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kugundua baadhi ya matatizo yanayowakabili vijana wetu sambamba na kuwapa elimu ya afya jinsi ya kulinda afya ya miili yao haswa misuli kwa kufanya mazoez kwa bidii na njia iliyo sahihi ili iwasaidie kufanya vizuri katika mechi zao za kila siku” alisema.


Vipimo ambavyo walifanyiwa nyota hao ni pamoja na vipimo vya damu kama vile blood group, blood glucose, blood pressure,Afya ya masikio, uoni wa macho, misuli pamoja na joints.

No comments:

Post a Comment