Chama cha mchezo wa
kikapu visiwani Zanzibar kipo katika mipango ya mwisho yakufanikisha uchaguzi
mkuu wa chama hicho.
![]() |
KIKOSI CHA TIMU YA KIKAPU YA AFRICAN MAGIC |
Akizungumza na
zenjsport-on line makamo mwenyekiti wa
chama cha mchezo wa mpira wa kikapu Zanzibar Rashid Hamza amesema harakati za
kufanikisha uchaguzi huo zinaenda vizuri.
![]() |
Uwanja_wa_mpira_wa_kikapu |
Ameongeza kuwa kwa
mujibu wa marekebisho ya katiba ya chama hicho kutakuwa na mapungufu ya baadhi
ya nafasi ambapo mwaka huu kutakuwa na nafasi chache sana zakugombania.
“Unajua tunachosubiri
sasa ni kutoka kwa katiba yetu mpya na katika mpya imepunguza idadi ya nafasi za
kugombania tofauti na zamani katiba iliyokuwa ikitumika nyuma ilikuwa na nafasi
ya makamo mwenyekiti Unguja na Pemba sambamba na naibu katibu Unguja na pemba
jambo ambalo katika katiba mpya nafasi hizo hakuna”alisema makamo mwenyekiti
huyo.
Aidha amevitaka vilabu
kulipia ada ya mwaka kwa baraza la michezo ilikufanikisha kushiriki katika
zoezi hilo la uchaguzi.
No comments:
Post a Comment