Kikosi cha mabingwa
wa mashindano ya vijana ya Rolling Stone kombain ya Mjini Unguja kimezidi
kuimarika baada ya kuongezeka kwa kiungo mshambuliaji wa timu ya taifa ya
vijana ya Tanzania Serengeti Boys na timu ya Kilimani City Assad Juma lengo
ikiwa ni kutetea taji walilotwaa katika msimu uliomalizika.
Kwa mujibu wa taarifa
iliyotolewa na mwalimu wa timu hiyo Muhammed Seif King amesema ameamua
kumuongeza kiungo huyo ilikuimarisha zaidi kikosi chake.
![]() |
DECO AKIWA MZIGONI |
Ukiachia Hussein Deco
nyota wengine walioitwa kuongeza nguvu katika kikosi hicho ni pamoja na
mshambuliaji wa Miembeni City ambae pia alikuwepo katika kikosi cha Serengeti
boys kilichokuwepo AFCON Ibrahim Abdallah(Imu Mkoko), mlinda mlango wa Miembeni
City Aley Ally,mshambuliaji wa Villa United Juma Ali Yussuf “James” na Muharami
Khamis “Terra” wa Black Sailors pamoja na Abdul hamid Salum “Ramos” KVZ.
Kikosi cha Mjini Unguja (Mabingwa watetezi) mpaka sasa kina
jumla ya nyota 26 wakiwemo walinda mlango Aley Ali Suleiman “Manula” (Miembeni
city), Peter Dotto Mashauri (Schalke 04) na Makame Mkadar Koyo (Huru).
![]() |
KIUNGO WA KILIMANI CITY ASAAD JUMA AKIWA NA MSHAMBULIAJI WA MIEMBENI CITY IBRAHIM ABDALLAH |
Wachezaji wa ndani ni
Muharami Khamis “Terra” (Black Sailors), Abdul hamid Salum “Ramos” (KVZ), Ali
Juma Maarifa “Mabata” (Taifa ya Jan’ombe), Hassan Chalii (Kipanga), Abdul-halim
Ameir (King Boys), Shaaban Pandu (Villa United), Idrissa Makame (Villa FC),
Ramadhan Simba (Calypso), Ali Hassan (Uhamiaji), Fahmi Salum (Mlandege), Salum
Omar (Villa United), Yakoub Omar (Jang’ombe Boys) na Mohd Ridhaa (Villa
United).
Wengine ni Mohd Jailan
(Chrisc), Makame Masoud (Schalke 04), Mohd Mussa (Mapembeani), Abrahman Juma
(KMKM), Mohd Haji (Jang’ombe Boys), Abdul-hamid Juma (ZAFSA), Ibrahim Chafu
(Villa FC) ,Ibrahim Abdallah(Miembeni Cit),Asaad Juma (Kilimani City)na Juma Ali
Yussuf “James” (Villa United).
KOCHA WA COMBINE YA WILAYA YA MJINI MUHAMED SEIF KING AKISALIMIANA NA KOCHA WA ZIMAMOTO SEIF BAUSI ALIEVAA FULANA CHEUPE |
No comments:
Post a Comment