Tuesday, 30 May 2017

BOYS WAZIDI KUJIFUA KWA AJILI YA MASHINDANO YA SPORT PESA

Timu ya Jang’ombe boys wanaendelea kujinoa kwa ajili ya mashindano ya Sport pesa super cup yanayotarajiwa kufanyika Tanzania bara mapema mwezi ujao .
KIKOSI CHA TIMU YA JANG'OMBE BOYS KITAKACHOSHIRIKI KATIKA MASHINDANO YA SPORT PESA


Akizungumza na zenjsport-on line kocha mkuu wa timu hiyo Mahmoud Abdallah Yussuf amesema vijana wake wapo katika hali nzuri huku akitarajia kufanya vyema zaidi katika mashindano hayo.

Aidha maeongeza kuwa vijana wake wapo katika ari kubwa kuona wanafanya vyema katika michezo hiyo huku akiamini kuwa watafanya vyema katika mashindano hayo.
ABDI KASSIM BABI AKIWA KATIKA MAJUKUMU YA JANG'OMBE BOYS.


Akizungumzia wapinzania wake kocha huyo amesema wanawaheshimu sana wapinzani wao na ni timu nzuri lakini anawaanda wachezaji wake kwa ajili yakupambana.

Kwa upande wake Abdi Kassim Babi amesema mazoezi yanaenda vizuri atatumia uzoefu alionao kuona timu inafanya vizuri katika michezo hiyo.
ABDI KASSIM BABI AKIWAJIBIKA NJE YA TANZANIA 


Amewataka wadau na washabiki wa soka visiwani Zanzibar kuunga mkono juhudi za timu yao ilikufanya vyema nakuijengea heshima Zanzibar kisoka.

No comments:

Post a Comment