Thursday, 22 June 2017

FEREJI SALUM AREJEA UWANJANI.

Kiungo wa timu ya Jang’ombe boys Ferej Salum(Ozil) amerejea uwanjani baada yakukaa nje kwa takribani miezi mitatu kuuguza majeraha ya goti.
Kiungo Ferej Salum wakati alipokuwa Villa United

Fereji ambae amesajiliwa Jang’ombe boys katika kipindi cha dirisha dogo akitokea Villa United nakushindwa kuitumikia timu yake hiyo mpya katika michezo ya ligi kuu kutokana na majeraha hayo aliyoyapata katika michezo yakujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu soka ya Zanzibar.

Kiungo huyo ambae alikuwa majeruhi ameanza kurudi uwanjani katika mchezo wa kirafiki kati ya timu ya combine ya Rolling Stone na timu yake mchezo ambao umefanyika usiku wakumkia leo na kuonesha kiwango cha hali ya juu.

Akizungumza na mtandao huu kiungo huyo ameeleza kuwa anafurahishwa na hali ya afya yake nakuwaomba wadau na wapenzi wa soka wazidi kumuombea ili hali yake iwe vizuri zaidi.
Ferej Salum akiwa katika picha ya pamoja na kikosi cha Azam B.

Ameongeza kuwa baada yakukaa juu kwa takribani miezi mitatu kwa sasa anatahakikisha anafanya mazoezi ya nguvu ilikurudisha kiwango chake nakuisadia timu yake kutwaa ubingwa wa ligi kuu soka ya Zanzibar.


Nyota huyo ambae pia alipitia katika kituo cha soka cha Azam amesema kwa sasa akili yake yote anaielekeza katika kurejesha kiwango chake nakuachana na kila aina ya anasa ilikufikia malengo ambayo amejiekea.

No comments:

Post a Comment