Timu ya JKU
inayoshiriki ligi kuu soka ya Zanzibar imepania kuona wanapata huduma ya kiungo
mshambuliji wa Miembeni City HarounAbdallah Jabir(Boban).
Boban ambae alikuwa
chachu ya mafanikio ya timu yake katika msimu uliomalizika wa ligi timu ikiwa
inashiriki ligi daraja la kwanza taifa nakufanikiwa kuipandisha ligi kuu amekuwa
akifuatiliwa na timu hiyo kwa kipindi kirefu sasa.
Akizungumza na mtandao
huu katibu wa JKU Saad Ujudi amesema mwalimu amependekeza jina la nyota huyo
tokea msimu uliopita lakini jitihada zakunasa saini ya nyota huyo ikashindikana
lakini bado wanahitaji huduma ya nyota huyo.
Ameongeza kuwa bench
la ufundi la timu yake wamependekeza tena jina la nyota huyo kujumuishwa katika
usajili wa msimu ujao wa ligi na tayari wameshatumwa watu kufuatilia suala
hilo kwa hatua ya awali.
“Tulimuhitaji nyota
huyu tokea msimu uliopita lakini ilishindikana kutokana na kuhitajika na timu
yake,na msimu huu pia mwalimu aliyopo amependekeza jina lake na sisi kama
uongozi tushaanza taratibu za awali zakufuatilia uwezokano wa nyota huyo
kujiunga na kikosi chetu”Alisema katibu huyo.
Mtandao huu umemtafuta
mkurugenzi wa ufundi wa timu ya Miembeni City, Ali Muhammad kujua kuwa tayari
kuna ofa yoyote ile kutoka kwa JKU nakusema mpaka sasa hakuna ofa yoyote ile
iliyokuja kutoka kwa timu hiyo.
Amefafanua kuwa JKU
waliwafata katika msimu ulimalizika kutaka kumchukua nyota huyo lakini
hawakufikia makubaliano kutokana na timu kumuhitaji nyota huyo.
Aidha ameweka bayana
kuwa timu yao inakaribisha mazungumzo na timu yoyote ile na endapo watafikia
makubaliano wapo tayari kumuachia nyota wao yoyote kuenda timu yoyote ile
inayomtaka.
No comments:
Post a Comment