Saturday, 24 June 2017

SURE BOY ANG’ARA ,MLANDEGE IKIIFUNGA TAIFA.

Mchezaji wa timu ya Azam FC Abuabakary Sure boy ametokea nyota wa mchezo(man of the match) katika mchezo wa ufunguzi wa mashindano ya Coconut FM Ndondo cup mtanange uliovurumishwa katika dimba la Amani mjini Unguja usiku wakuamkia leo.
Kikosi cha Mlandege 

Mtanange huo ambao ulikuwa na ushindani na mvuto kwa washabiki waliofika uwanjani hapo huku ukishuhudiwa na mlinzi  wa Liverpol ya England Mamadou Sakho ulikuwa na ushindani wa hali ya juu.

Katika mchezo huo ambao umeshuhudiwa na mashabiki kadhaa magol ya Mlande yalifungwa na Abdallah Edi Mundo dakika ya 60 na Razak Halfan dakika ya 78.

Huku goli pekee la Taifa limekifungwa na Ali Badru dakika ya 30.


Mashindano ya Coconut Ndondo Cup yanatarajiwa kuendelea baada yakumalizika sherehe za Idd.

No comments:

Post a Comment