Saturday, 24 June 2017

NINAENDA YANGA KUPAMBANA ,NINJA.


Mlinzi mpya wa timu ya Yanga Abdallah Haji Shaibu "Ninja" amesema mara baada yakufanikiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na timu ya Yanga ya Dar es salam kwa sasa anajipanga kuona anapata namba ya uhakika katika kikosi hicho chenye maskani yake katika mtaa wa Jangwani.

Ninja ameyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na zenjsport -on line nakusema anajua atakabiliana na changamoto katika kikosi hicho lakini atahakikisha anajituma ili awe chaguo namba moja la kocha wa kikosi chake hicho kipya.
 
Abdallah Haji Shaibu "Ninja"
Amesema moja ya ndoto zake nikucheza katika timu kubwa lakini kufika kwake yanga ni miongoni mwa njia zakufikia kule alikojipangia.
 “Yanga ni kama njia kwangu yakusonga mbele zaidi lengo langu nikucheza soka nje ya Tanzania naamini kujituma kwangu ndiko kutakakosaidia kufikia malengo yangu “Alisema Ninja.

Aidha nyota huyo amewaomba mashabiki wa soka visiwani na wapenzi wake kumuombea dua ilikufanikisha malengo yake aliyojiekea nakusema kuwa atahakikisha anapambana ipasavyo ilikufikia malengo yake.


Ninja ndie mchezaji wa kwanza msimu huu wa mwaka 2017-2018 kusajiliwa Yanga akitokea Taifa ya Jang’ombe ya Zanzibar ambapo amefunga mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment