Kocha mkuu wa timu ya
Mwadui ya Shinyanga Ali Bushir Mahmoud amewataka viongozi wa chama cha mpira wa
miguu visiwani kubadilika kiutendaji ilikuimarisha soka katika visiwa vya
Zanzibar.
Bushir ametoa ushauri
huo wakati alipokuwa akizungumza na zenjsport on line nakusema kuwa baada ya
Zanzibar kupata uanachama wa shirikisho la soka barani Afrika (CAF) lazima viongozi wa chama cha soka kubadilika
kiutendaji nakuacha kufanya kazi kimazoea ilikukuza soka la Zanzibar.
“Lazima tujieke sawa
katika uongozi,tuache ubabaisha katika kuongoza soka hapa ndani lazima
tujirekebishe tufanye soka la nyumbani liwe la ushindani na tuwe na nizamu
sambamba na kuwa na watu wa mpira kweli ambao watafata kanuni na sheria
zinazoongoza soka”Alisema Bushir.
Amesema kuwa umefika
wakati sasa kwa Zanzibar kutengeneza katiba ambayo itakuwa imara na yenye
kuangalia masilahi ya soka la Zanzibar nakuwataka viongozi wa vilabu kuwa na
viongozi wanaongoza vilabu vyao wenye uweledi wakuendesha shughuli za mchezo wa
soka ilikuendesha timu zao katika misingi iliyoimara.
Akizungumzia soka la
vijana kocha huyo amewataka viongozi wa ZFA kuandaa mfumo nzuri ambao utasaidia
kukuza soka la Zanzibar nakupelekea kuwa na timu za taifa imara katika miaka
mitano ijayo.
No comments:
Post a Comment