Tuesday, 13 June 2017

Ndondo Cup zichezwe baada yakumalizika kwa ligi ilikunusu vipaji vya wachezaji wetu..asema kocha King



Kocha mkuu wa timu ya combine ya wilaya ya mjini Unguja ambayo itashiriki katika michezo ya rolling stone Muhamed Seif King amewataka wadau wa soka wanaoanzisha mashindano ya ndondo cup kuanzisha michezo hiyo kipindi ambacho ligi zitakuwa zimemalizika.
 
Aliyekuwa kocha wa timu ya Miembeni City,Jang'ombe na JKU Muhamed Seif King.
Kocha king ameyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na mtandao huu ambao ulitaka kujua sababu ambayo inamfanya kuwazuia nyota ambao wapo katika kikosi chake wasishiriki katika mashindano hayo ya Ndondo Cup kila yanapoanzishwa.

Amesema kuwa mashindano ya Ndondo ni mashindano mazuri kwani yanaongeza ukomavu kwa wachezaji lakini utaratibu wakuanzishwa mashindano hayo katika kipindi cha ligi inaendelea ndiko kunakoharibu mashindano hayo.

“Kwanza nataka nikuambie mimi ni muumini wa mashindano hayo ya Ndondo kwa sababu ili mchezaji apate ushindani na ukomavu lazima amepitia katika yale mashindano lakini ligi inaendelea huku mashindano yale yanaendelea hivyo yanamfanya mchezaji achoke jambo ambalo linapelekea wachezaji wetu wanachoka mapema “alisema kocha huyo.

Akizungumzia soka la Zanzibar kocha huyo amesema visiwa hivi vimebarikia vipaji vya soka hususani katika kada ya vijana jambo ambalo linapelekea kufanya vyema katika mashindano mbalimbali ya vijana ambayo Zanzibar inashiriki.

Ameongeza kuwa Zanzibar ni brazil ya afrika mashariki kwa kuzalisha vipaji lakini tatizo la umasikini ambalo linawakabili vijana wengi wenye vipaji ndilo kunakopelekea kufifia vipaji vyao katika umri mdogo.

Aidha amesema wanaenda katika mashindano ya Rolling Stone kutetea taji ambalo walitwaa katika mashindano ambayo yamepita.

No comments:

Post a Comment