Katibu mkuu
wa mashindano ya vijana visiwani Zanzibar Abdallah Thabit (Dulla Sunday)
amewataka vijana kuitumia fursa ikiyopo sasa katika kushiriki katika mchezo wa
soka la ufukweni.
![]() |
WACHEZAJI WA SOKA LA UFUKWENI WAKIWA KATIKA MCHEZO HUO. |
Ushauri huo
ameutoa wakati alipokuwa akizungumza nasi nakusema kuwa endapo vijana
watashiriki katika mchezo huo utawasaidia kujitangza kupitia mchezo huo ambao
kwa kwa sasa umekuwa ukipewa kipaumbelea na shirikisho la soka barani Afrika
sambamba na FIFA.
Ameongeza kuwa
ushiriki katika mchezo huo wa soka la ufukweni utasaidia kwa baadhi ya vijana
ambao wameshindwa kushiriki kimataifa kupita michezo mengine kuonesha uwzo wao
nakushiriki kimataifa.
Aidha katibu
huyo amewataka wadau mbalimbali wa soka nchini kuungana na kamati inayosimamia
mipira wa ufukweni ilikuimarisha mchezo huo nakutoa nafasi kadhaa kwa vijana wa
kizanzibar kuonesha vipaji ambavyo wanavyo.
No comments:
Post a Comment