Sunday, 9 July 2017

Mjini waanza vyema kampeni za kutetea taji Manyara.

Mabingwa watetezi wa Mashindano ya Vijana ya Afrika Mashariki na Kati ya Rolling Stone timu ya Kombain ya Mjini Unguja wameanza vyema kampeni za kulitetea taji walilotwaa mwaka jana baada ya kuwafumua wenyeji wao timu ya Mbulu All Stars mabao 4-0 mchezo uliopigwa katika uwanja wa Julius Nyerere huko Mbulu Mkoani Manyara.
 
Wachezaji wa combine ya wilaya ya mjini.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani kwa pande zote magoli ya washindi yalifungwa na Mohd Vuai “Prince”, Seif Said “Tiote”, Abdul hamid Juma (Samatta) na Fahmi Salum (Migwel).
 
kikosi cha mbulu all star.
Kikosi kilichoanza cha combine ya wilaya ya mjini katika mchezo wa jana ni George Munish,Hassan Chalii,Muharami Khamis,Abubakary Ame,Ali Juma,Muhamed Yahya ,Abrahaman Juma,Yakoub Amour,Muhamed Vuai,Ibrahim Abdallah,Seif Said.
Sub .
Ali Mbarouk,Muhamed Jailan,Mohamed Haji,Suleiman Ali,Fahmi Salum,Abdulhamid Juma na Muhamed Chafu

Mjini watashuka tena Dimbani siku ya Jumanne ya July 11, 2017 kucheza na  Kenya saa 8:00 za mchanakatika uwanja wa Julius Nyerere huko Mbulu Mkoani Manyara.


No comments:

Post a Comment