Sunday, 16 July 2017

RUVU SHUTING KUONDOKA NA NYOTA WAWILI ZANZIBAR.

Katika kuhakikisha wanakiimarisha kikosi chao kwa ajli ya msimu ujao wa ligi timu ya Ruvu shuting ipo visiwani Zanzibar kusaka nyota wataowasajili kwa ajili ya kuitumikia timu hiyo.
Masau Bwire msemaji wa Ruvu Shuting

Akizungumza na mtandao huu akiwa kisiwani Unguja msemaji wa timu hiyo Masau Bwire amesema amekuja kuangalia vipaji vya wachezaji wa Zanzibar na kusema tayari wapo katika mazungumzo na baadhi ya wachezaji na endapo watakubaliana anatarajia kuondoka na nyota hao.

Amongeza kuwa tayari uongozi wa timu hiyo wapo katika mazungumzo na nyota wawili kutoka Unguja na endapo watafikia makubaliano nyota hao watasaini mkataba wakujiunga na kikosi chao hicho.
Masau Bwire

Amefafanua kuwa wanahitaji vijana wenye umri mdogo kwani wanataka kukijenga kikosi chao hicho kwa miaka minne ijayo.


Aidha amesema kuwa ni mapema sana kuwataja ni kina nani hao ila watakapofikiana makubakilano wataweka bayana ni akina nani hao ambao wataitumikia timu hiyo kwa msimu ujao.

No comments:

Post a Comment