Aliyekuwa kocha wa timu ya Mwadui FC inayoshiriki ligi kuu soka ya
Vodacom Tanzania bara Ali Bushir amekuwa akifuatiwa kwa karibu na timu ya
Muembeladu inayoshiriki ligi daraja la pili wilaya ya mjini Unguja.
![]() |
Kocha Ali Bushir wa kwanza alieva kapelo akiwa katika moja ya michezo ya Kagame wakati akiifundisha KMKM. |
Muembeladu ambayo iliwahi kupata huduma ya mwalimu huyo huko nyuma
imepania kuona wanapata huduma ya kocha huyo ilikukinoa kikosi chao hicho. Akizungumza
na mtandao huu msemaji wa timu hiyo Said Mussa amesema uongozi wa timu hiyo
tayari umeshafanya mazungumzo na mwalimu huyo na mazungumzo yameenda vizuri.
Amesema kuwa lengo la timu yao nikuona inapanda daraja na ilikufikia
lengo lao hilo walilojiekea wakaona umuhimu wakutafuta mwalimu ambae anauwezo
nakufanikisha lengo lao hilo.
Kwa upande wake kocha Ali Bushir amesema ni kweli amefanya mazungumzo na
uongozi wa timu hiyo na anajipanga kufanya kazi na uongozi wa timu hiyo kwa
mujibu wa makubaliano yao.
Amesema ataenda kuisaidia timu hiyo kwa vile mipango yake nikufundisha
soka Tanzania bara lakini kutokana na mipango yake yakuenda huko haijakaa
vizuri ameamua kutumia muda wake aliopo hapa mkuwasaidia vijana hao.
Licha ya Muembeladu kocha huyo amekuwa akihitajiwa na timu kadhaa
visiwani hapa lakini ameshinda kufanya nao mazungumzo kutokana na malengo yake
nikuenda kufundisha soka Tanzania bara.
No comments:
Post a Comment