Wednesday, 30 August 2017

MUEMBELADU YANYEMELEA HUDUMA YA BUSHIR

Aliyekuwa kocha wa timu ya Mwadui FC inayoshiriki ligi kuu soka ya Vodacom Tanzania bara Ali Bushir amekuwa akifuatiwa kwa karibu na timu ya Muembeladu inayoshiriki ligi daraja la pili wilaya ya mjini Unguja.
 
Kocha Ali Bushir wa kwanza alieva kapelo akiwa katika moja ya michezo ya Kagame wakati akiifundisha KMKM.
Muembeladu ambayo iliwahi kupata huduma ya mwalimu huyo huko nyuma imepania kuona wanapata huduma ya kocha huyo ilikukinoa kikosi chao hicho. Akizungumza na mtandao huu msemaji wa timu hiyo Said Mussa amesema uongozi wa timu hiyo tayari umeshafanya mazungumzo na mwalimu huyo na mazungumzo yameenda vizuri.

Amesema kuwa lengo la timu yao nikuona inapanda daraja na ilikufikia lengo lao hilo walilojiekea wakaona umuhimu wakutafuta mwalimu ambae anauwezo nakufanikisha lengo lao hilo.

Kwa upande wake kocha Ali Bushir amesema ni kweli amefanya mazungumzo na uongozi wa timu hiyo na anajipanga kufanya kazi na uongozi wa timu hiyo kwa mujibu wa makubaliano yao.


Amesema ataenda kuisaidia timu hiyo kwa vile mipango yake nikufundisha soka Tanzania bara lakini kutokana na mipango yake yakuenda huko haijakaa vizuri ameamua kutumia muda wake aliopo hapa mkuwasaidia vijana hao.

Licha ya Muembeladu kocha huyo amekuwa akihitajiwa na timu kadhaa visiwani hapa lakini ameshinda kufanya nao mazungumzo kutokana na malengo yake nikuenda kufundisha soka Tanzania bara.


No comments:

Post a Comment