Saturday, 26 August 2017

TUTAHAKIKISHA TUNAZIFANYIA KAZI KASORO ZILIZOJITOKEZA MSIMU ULIOPITA,MZIRAI.

Kamati inayosimamia mashindano ya vijana ndani ya wilaya ya mjini Unguja imejipanga kuona wanazifanyia kazi changamoto zilizojitokeza katika mashindano ya msimu uliopita ili zisijirejee tena katika msimu mpya wa mashindano hayo.

Hayo yameelezwa na mshika fedha wa kamati ya mashindano ya vijana ndani ya wilaya hiyo Mussa Habibu Mzirai wakati alipokuwa akizungumza na mtandao huu nakusema katika mashindano yaliyomalizika kulikuwa na kasoro kadhaa ambazo zimepelekea kutia dosori mashindano hayo.

Amesema moja ya changamoto ambazo kamati yake imekabiliana nazo katika msimu uliopita ni pamoja na vitendo vya upangaji wa matokeo,mashindano kutokumalizika kwa wakati na uhaba wa viwanja jambo ambalo kamati yao kwa msimu 2017-2018 itahakikisha changamoto hizo hazijitokeze.

Akizungumzia suala la upangaji wa matokeo Mzirai amesema vitendo hivyo vilijitokeza mwishoni mwa mashindano ya Central nakuahidi kutoa adhabu kali kwa yoyote yule atabaaini na vitendo hivyo katika msimu ujao.

Kuhusu zoezi la uhamisho na usajili linaloendelea amesema zoezi hilo linaenda vizuri huku muamko wa vilabu ukionekana kuwa mkubwa.


Amewaomba wadau wa wapenzi wa mchezo wa mpira wa miguu kujitokeza kuunga mkono jitihada za kamati yao ilikuyafanya mashindano hayo yawe na mvuto na ushindani zaidi.

No comments:

Post a Comment