Kocha mkuu
wa timu ya Miembeni City Muhamed Seif King ametoa mapumziko ya siku tano kwa
wachezaji wa timu hiyo ilikutoa nafasi kwa nyota hao kusherehekea skukuu ya ld
el hajj ambapo waislam wote ulimwenguni waatarajiwa kusherehekea hapo kesho.
![]() |
Kocha mkuu wa timu ya Miembeni City Muhamed Seif King akizungumza na nahodha wa timu hiyo Habibu |
King ametoa
mapunziko hayo baada ya ushindi wa magol 4-1 dhidi ya Chuoni ikiwa ni miongoni
mwa michezo ya kirafiki kwa timu hiyo ambayo ipo katika kujiandaa kwa ajili ya
msimu wa 2017-2018 ligi kuu soka ya Zanzibar.
Akizungumza na
wachezaji hao kocha huyo amesema wamecheza michezo mitatu ya kirafiki lengo kuu
kwake nikuangalia mfumo ngani anaweza kuutumia katika kikosi chao hicho ambacho
kimesheni nyota vijana na wenye uwezo wakusakata kabumbu.
Amesema michezo
hiyo imemuonesha mapungufu ambayo vijana wake wanayo na atahakikisha
anayafanyia kazi ilikuwa na kikosi
kilicho imara na bora.
Miembeni City
ambayo itashiriki kwa mara ya kwanza ligi kuu soka ya Zanzibar imecheza michezo
mitatu ya kirafiki ambapo waliifungwa Mchangani magol 3-0,wakatoka sare ya goli
1-1 na timu ya New King nakuibuka na ushindi wa magol 4-1 dhidi ya Chuoni
wanatarajiwa kurudi mazoezi Jumatatu Sepember 4 kuendelea kujiandaa na msimu
ujao wa ligi.
No comments:
Post a Comment