Thursday, 31 August 2017

Miembeni City ,mapumzikoni hadi September 4.

Kocha mkuu wa timu ya Miembeni City Muhamed Seif King ametoa mapumziko ya siku tano kwa wachezaji wa timu hiyo ilikutoa nafasi kwa nyota hao kusherehekea skukuu ya ld el hajj ambapo waislam wote ulimwenguni waatarajiwa kusherehekea hapo kesho.
Kocha mkuu wa timu ya Miembeni City Muhamed Seif King akizungumza na nahodha wa timu hiyo Habibu 

King ametoa mapunziko hayo baada ya ushindi wa magol 4-1 dhidi ya Chuoni ikiwa ni miongoni mwa michezo ya kirafiki kwa timu hiyo ambayo ipo katika kujiandaa kwa ajili ya msimu wa 2017-2018 ligi kuu soka ya Zanzibar.

Akizungumza na wachezaji hao kocha huyo amesema wamecheza michezo mitatu ya kirafiki lengo kuu kwake nikuangalia mfumo ngani anaweza kuutumia katika kikosi chao hicho ambacho kimesheni nyota vijana na wenye uwezo wakusakata kabumbu.

Amesema michezo hiyo imemuonesha mapungufu ambayo vijana wake wanayo na atahakikisha anayafanyia kazi  ilikuwa na kikosi kilicho imara na bora.


Miembeni City ambayo itashiriki kwa mara ya kwanza ligi kuu soka ya Zanzibar imecheza michezo mitatu ya kirafiki ambapo waliifungwa Mchangani magol 3-0,wakatoka sare ya goli 1-1 na timu ya New King nakuibuka na ushindi wa magol 4-1 dhidi ya Chuoni wanatarajiwa kurudi mazoezi Jumatatu Sepember 4 kuendelea kujiandaa na msimu ujao wa ligi.

No comments:

Post a Comment