Timu
ya Black Sailors inayoshiriki ligi kuu soka ya Zanzibar imeijia juu timu ya
Ndanda FC ya Mtwara inayoshiriki ligi kuu soka ya Vodacom Tanzania bara kwa
kumtumia mchezaji wao Majid Khamis Bakar "Dudu" bila ya kufata
taratibu za usajili.
Ndanda walimtumia mchezaji
huyo katika mchezo wao wa kwanza wa ligi kuu soka Tanzania bara mchezo ambao
walipokea kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Azam FC ambapo mchezaji huyo alicheza
takribani dakika 75 akiwa amevalia jezi nambari 12 , namba ambayo alikuwa
akiitumia akiwa Black Sailors.
Akizungumza na mtandao
huu katibu mkuu wa timu ya Blacksalor Issa Hatibu Masiku amesema utaratibu wa
uhamisho wa nyota huyo haujafanyika kutoka kwao na nyota huyo amesajiliwa pia
katika timu yao.
Amesema mazungumzo ya
awali kwa pande hizo mbili yalifanyika lakini makubaliano hayakufikiwa lakini
Ndanda wakaamua kumtumia nyota huo bila yakufuata taratibu za uhamisho.
“Unajua tulifanya
mazungumzo ya awali na Ndanda lakini lakushangaza taratibu za uhamisho
hazijafanyika nyota huyo ameweza kutumika katika mchezo wao dhidi ya Azam”alisema
katibu huyo.
Ameongeza kuwa timu yao
itafata taratibu kuona wanapatia haki stahiki huku akiviomba vyama vya mpira wa
miguu nchini kuzingatia sheria na kanuni zinafatwa katika kipindi cha usajili
na uhamisho.
No comments:
Post a Comment