Friday, 10 November 2017

BUSHIR KUONGEZA NGUVU CHARAWE.

Kufuatia kucheza michezo mitano nakupoteza katika michezo yote  uongozi wa timu ya Charawe imemteua kocha Ali Bushir kukinoa kikosi chao hicho katika michezo iliyosalia.


Hayo yamethibitishwa na katibu wa timu hiyo Haji Bakar wakati alipokuwa akizungumza nasi nakusema wana imani kubwa kocha huyo anaisadia timu yake ifanye vyema.

Amesema kuwa anamatumaini makubwa timu itafanya vyema kufuatia ujio wa kocha huyo ambae amekuwa na uzoefu katika ligi kuu ya Zanzibar.

Ameongeza kuwa kocha huyo amekubali kufanya kazi katika kikosi hicho nakuahidi kutoa mashirikiano ya hali ya juu katika kikosi chao hicho.


Charawe ambayo inashiriki kwa mara ya kwanza ligi kuu soka ya Zanzibar tayari imeshacheza michezo mitano nakupoteza katika michezo yote mitano.

No comments:

Post a Comment