Hatimae ligi kuu ya
netball iliyokuwa ifanyike kisiwani Pemba yaota mbawa kutokana na ukata wa
fedha unaovikabili vilabu sambamba na chama cha mchezo huo.
Hayo yameelezwa na
katibu wa chama cha mchezo huo Said Ali mansab wakati alipokuwa akizungumza na
mtandao huu.
Amesema chama chao
kimepokea taarifa kutoka kwa wenzao waliopo Pemba kuwa vilabu vya Pemba
havitashiriki katika ligi hiyo nakupelekea viongozi kukutana hapo jana kujadili
suala hilo nakutafuta njia ya kufanya ilikupatikana muwakilishi wa Zanzibar
katika ligi ya Muungano.
Aidha ameongeza kuwa
baada yakukutana chama cha netball Zanzibar kimeamua vlabu vya Unguja kushiriki
katika kombe la Muungano sambaba na mashindano ya Afrika mashariki na kati
yatakayofanyika mwezi wan ne mwakani.
Akivitaja vilabu
vitakavyoshiriki katika ligi hiyo ya Muungano katibu huyo amesema ni pamoja na
JKU,Mafunzo,Duma ,KVZ,Zimamoto na Afya.
Amewataka wadu wa
mchezo huo kuwaunga mkono ilikuimarisha mchezo huo visiwani hapa.
Ligi kuu ya Muungano
kwa mchezo wa Net ball inatarajiwa kufanyika kuanzia November 26 mwaka huu
katika kiwanja cha Gymkhana.
No comments:
Post a Comment